
Serikali kupitia Wizara ya Ardhi,
Nyumba na Maendeleo ya Makazi imedhamiria kutatua tatizo la wawekezaji katika
ardhi na mashamba
wasiokuwa na dhamira njema na
maendeleo ya nchi hii.Hili limejidhihirisha dhahiri katika zoezi linaloendelea
la kubaini maeneo husika na kuyabatilisha kutoka kwa wamiliki husika na kupatiwa
wananchi kuyaendeleza sambamba na agizo la Mheshimiwa Rais John Pombe Magufuli.Hivi
karibuni, Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi; Mheshimiwa William Lukuvi
alizitaka halmashauri zote nchini, kufanya uhakiki wa mashamba makubwa ambayo hayajaendelezwa
kwa muda mrefu na kutoa notisi kwa wamiliki wake ili wafahamu hatua zitakazochukuliwa
na Serikali.Alisema hayo wakati akitangaza kwa wananchi wa Tanga kuhusu kufutwa
kwa hati miliki ya mashamba matano ya mkonge yaliyopo wilaya za Muheza na
Pangani. Mashamba hayo ni Lewa Estate, Kipumbwi, Azimio, Bwembwera na
Sakula.Mheshimiwa Lukuvi alisema;
“Mheshimiwa Rais alifikia uamuzihuo Desemba 19, mwaka jana baada ya kujiridhisha
kuwa wamiliki wake wameshindwa kuyaendeleza mashamba hayo kwa shughuli
zilizokusudiwa kama walivyokuwa wameomba katika vijiji husika”.Mheshimiwa
Lukuvi aliuagiza mkoa wa Tanga, upendekeze mali zilizopo kwenye mashamba hayo,
kama majengo ya ofisi na mali nyingine
wapewe watu gani kwa ajili ya
maendeleo ya eneo husika kabla mashamba hayo hayajagawiwa.
Pia, aliagiza kuwa mkoa lazima
uhakikishe wamejua idadi kamili ya wananchi walioko katika mashamba hayo na
kiasi cha ardhi iliyopo, ikiwepo kufanya utaratibu pia wa ulipaji wa fidia kwa
wale
wanaostahili.Aidha, amani
iliyokosekana kwa takriban miaka kumi katika Kijiji cha Kapunga wilayani
Mbarali mkoa wa Mbeya, imerejea baada ya Mheshimiwa Lukuvi kuwatangazia wananchi
kurejeshwa kwa hekta 1,870 zilizounganishwa kimakosa kwenye shamba la mwekezaji
mwaka 2005. Awali mwaka 1985, Rais wa Serikali ya Awamu ya Kwanza, Mwalimu
Julius Nyerere, aliwaomba wakazi wa Kijiji cha Kapunga eneo lenye ukubwa wa
hekta 5,500 ili kupata eneo kwa ajili ya kilimo cha umwagiliaji, na hasa
kuboresha kilimo nchini. Wananchi walikubali ombi hilo la Mwalimu Nyerere na
kutoa hekta hizo. Lakini, wananchi hao
wa Kapunga walishangazwa baadaye
kuona kuwa hata yale maeneo waliyobaki nayo, yakafanywa kuwa ya mwekezaji
ambaye ni Kampuni ya Export Trading Group, Katika kipindi hicho chote cha miaka
kumi,
wananchi wa Kapunga wamekuwa
wakipata matatizo ya aina mbalimbali katika eneo hilo, kwa Export Trading Group
kujichukulia maeneo mengine ya
wananchi hao. Baadhi ya mateso
waliyopata kutoka kwa mwekezaji huyo
ni kuvunjiwa daraja, kumwagiwa sumu katika mashamba yao n.k.
Hatahivyo baada ya agizo la Rais la kumtaka mwekezaji
huyo, kurejesha kiasi cha hekta 1,870wa wananchi, maeneo hayo sasa ni ya
wananchi.
Mheshimiwa Lukuvi alitangaza;
“Tumekaa na kukubaliana, kiasi hiki cha ardhi kirejeshwe kwenu na mwekezaji
amekubali hekta hizo sasa ni mali ya kijiji chenu”.Zoezi limeendelea katika
mikoa ya Morogoro na Tanga, ambapo hati za miliki za mashamba makubwa 13 yenye
zaidi ya ekari 24,000, yaliyoagizwa na Mheshimiwa Rais Magufuli, zilifutwa na
mashamba hayo kukakabidhiwa kwa wananchi wasio na ardhi. Serikali imetakiwa
itenge maeneo mengine kwa ajili ya uwekezaji katika mikoa
hiyo, baada ya wamiliki wake
kushindwa
kuyaendeleza.Mheshimiwa Lukuvi
alisema: “Sheria ya vijiji inaruhusu vijiji kumilikisha ardhi isiyopungua ekari
50 kwa kuitisha mkutano wa kijiji ili uridhie, lakini baadhi ya viongozi wamekuwa
wakishirikiana na wawekezaji matapeli ili wapewe ardhi kwa njia za hila”.
Vile vile akiwa wilayani Monduli
mkoa wa Arusha, Mheshimiwa Lukuvi alikabidhi ekari 39,924 za mashamba kwa
wananchi, baada ya Mheshimiwa Rais Magufuli kufuta hatimiliki za wawekezaji 13.
Akiongea na wananchi wa kata za
Lokisale na Olmoti katika mkutano wa hadhara, Mheshimiwa Lukuvi alisema; “Rais
amefikia hatua hiyo baada
ya wawekezaji hao kushindwa
kuyaendeleza
mashamba waliyokabidhiwa kwa ajili
ya kilimo cha biashara na kuwaacha wananchi bila ardhi”. Kwa ujumla, Wizara ya
Ardhi inaendelea
kushughulikia umilikishaji ardhi
usiofuata sheria katika maeneo mengi nchini. Mathalani, katika wilaya ya
Simanjiro mkoa wa Manyara, wanakijiji wa Kilombero Kata ya Shambarai,
wamerudishiwa ekari 828 za mashamba manne yaliyochukuliwa na familia moja baada
ya kujimilikisha bila kufuata sheria. Familia ya watu wanne wa kijiji hicho,
walijimilikisha ekari 1,028 bila
kufuata kanuni, taratibu na sheria za ardhi, hivyo wananchi hao wakawanyang’anya
ekari 828 na kuwaachia ekari
200.Aidha, zaidi ya mashamba 35
yanatarajiwa
kubatilishwa milki na Serikali ndani ya mwaka
huu 2016.Source;: www.ardhi.go.tz
No comments:
Post a Comment