Thursday, 22 September 2016

MUONGOZO WA UPANGAJI, UPIMAJI NA UMILIKISHAJI ARDHI

Image result for picha za upangaji ardhiImage result for picha za upangaji ardhi


1.UPANGAJI WA ARDHI 
(SPATIAL PLANNING/URBAN PLANNING)
Maana ya upangaji wa Ardhi ni pamoja na uandaaji wa michoro ya ubunifu ya mipango miji ya maeneo ambayo itaratibu uendelezaji wa mji husika.(inaitwa town planning drawings inshort TP), Kubadilisha matumizi ya ardhi ya viwanja ambavyo vimeshapewa hati,  Kutoa vibali vya ujenzi wa majengo, Kutoa vibali vya upimaji wa Ardhi, Kufanya marekebisho ya michoro ya mipango miji Mchoro wa mipango miji ambao unaonyesha matumizi mbali mbali ya eneo husika e.g shule, open spaces etc ukishatayarishwa na manispaa ni lazima upelekwe wizarani kwa mkurugenzi wa mipango miji wa wizara ya ardhi ili audhinishe.
Pia kitengo hiki cha upangaji kimeboreshwa Zaidi kwa kushirikisha sekta binafsi katika upangaji na uboreshaji wa miji nchi, hata hivyo sekta binafsi zmeweza kuisaidia serikali katika kuboresha miji mingi hapa nchini kwa kuandaa mipango kabambe(master plan) katika mikoa mbalimbali na hivyo kuongeza mazingatio katika uendelezaji wa miji nchi kote

2.    UPIMAJI ARDHI (LAND SURVEYING)
 Maana ya upimaji Ardhi ni pamoja na kuweka mawe yan Beacpon na kuonyesha mipaka ya maeneo yalio pimwa ,
Kazi kubwa ya mpimaji ni kupima eneo ambalo tayari lina mchoro wa mipango miji na anatakiwa kupima kulingana na mchoro wa mipango miji kama unavyo eleza na kazi hii hufuata baada ya upangaji kukamiliaka yaani uandaaji wa mchoro(TP) wa eneo husika.
Upimaji huendana na mambo yafuatayo
·       Kupanda mawe(beacons)
·        Kutoa namba ya kiwanja/ eneo lililopimwa(plot number)
·        Kuonyesha ukubwa wa eneo (plot area)
·       Kuonyesha mipaka ya kiwanja(plot boundaries)
·       Kuandaa Ramani ya upimaji inayo onyesha mawe ya kiwanja, kiwanja namba, ukubwa wa kiwanja na mipaka ya kiwanja ambayo lazima iwe imesajiliwa na kuidhinishw na mkurugenzi wa upimaji na ramani wa wizara ya Ardhi

3.     UMILIKISHAJI WA ARDHI
Jukumu hili hufanywa na kitengo cha maafisa Ardhi kwa kushirikiana na Tume ya umilikishaji Ardhi kanda kwa niaba ya wizara ya Ardhi, pia kitengo cha umilikishaji Ardhi kina kazi ya Kuandaa hati miliki ya viwanja ambavyo vimeshapimwa na ili aanze kukuandalia hati utatakiwa umpelekee mchoro wa mipango miji unaonyesha kiwanja chako ili ajue matumizi yake, ramani ya upimaji ya kiwanja chako ili ajue anaanda hati ya kiwanja gani, kipo wapi na kina ukubwa gani hii husaidia wanapokadiria kodi ya kiwanja lazima wajue ukubwa wa kiwanja, Kazi nyingine ya kitengo hiki ni kuhuisha miliki yani kuongeza mda wa umilikiwa ardhi mana kuna hati za miaka 33, 66 na 99. Kazi nyingine ni kuhamisha miliki kutoka kwa mmiliki mmoja na kwenda kwa mwingine inaitwa transfer. Hati nayo ikisha kamilika kuandaliwa na manispaa au halmashauri ni lazima ikahakikiwe na kamishna wa ardhi wa Kanda kwa niaba ya wizara na hatimaye msajili wa hati naye ataisajili.

 mara nyingi gharama za kufanya yote hayo kwa sekta binafsi zinategemea wingi wa watu wanaohitaji kupangiwa na kupimiwa maeneo yao hata hivyo kwa makubaliano kati ya mteja na kampuni husika, wizara ya Ardhi kupiatia bodi ya mipango miji imeidhinisha makampuni 33 mpaka kufikia mwezi Agast, 2016 yatakayo shiriki kupanga miji na kufikia malengo ya kutoa hati nyingi Zaidi mpaka kufikia mwaka 2025.

No comments:

Post a Comment