UTANGULIZI
Makazi holela ni aina ya maendeleo ya ardhi yasio fuata utaratibu maalum ulio panga eidha na serikali au kikundi cha watu fulani,
Aina hii ya maendeleo ya ardhi ilianza mara tu baada ya binadam kuanza maisha ya kujitafutia chakula na malazi, hata hivyo kwa historia kipindi hicho cha binadam kuanzisha makazi ni mara baada ya ugunduzi wa moto na baadae ugunduzi chuma.
Hata hivyo, upembuzi yakinifu kuhusu maendeleo holela ya matumizi ya ardhi huja kutokana na kukosekana kwa usimamizi wa taratibi maalum za mipango ya matumizi bora ya ardhi na hii imetokea maeneon mbalimbali katika nchi nyingi duniani.
MAKAZI HOLELA KATIKA BARA LA ULAYA
Maendeleo holela ya ardhi katika bara la ulaya yalikua kwa kasi kubwa kipindi cha mapinduzi ya viwanda miaka ya 1850 na hata kupelekea kuanza kwa taaluma ya upangaji wa mitaa ili kuboresha hali ya makazi ya bara hilo, pia hali hiyo ilizidi kuongezea katika mabara mengine likiwemo bara la Africa.
kutokana na kukua na kuongezeka kwa uhitaji wa makazi ya wanachi katika nchi mbalimbali barani Afrika, ikiwemo Tanzania, kulipelipelekea ongezeko kubwa la ujenzi usio rasmi yani makazi holela, ambayo kwa namna moja au nyingine yameongeza kasi ya matumizi ya ardhi nchini
Nikirudi katika maana halisi ya makazi holela nchini, makazi holela yamekua yakiongezeka kadili siku zinavyozidi kwenda mbele
Maeneo yenye Makazi holela mara nyingi hua na huduma duni za jamii kama vile Zahanati, shule, maji, barabara, mifereji ya maji taka na maeneo ya utunzanji taka ngumu, lakini pia yamekua na nyumba zilizo chini ya kiwango na hatarishi kwa uhai wa wakazi wa nyumba husika, wakati mwingine makazi haya yanatokea katika maeneo yasio salama kwa maisha ya binadamu kama vile pembezoni mwa mito au milima ambayo hua inaporomoka mara tu inapopatwa na majimaji kipindi cha mvua, ikumbukwe maafa mengi hutokea kwa wakazi wa maeneo haya na kugharimu maisha au gharama kubwa ya serikali katika kusaidia jamii na kaya zilizo athirika.
SHUGHURI ZA KIUCHUMI KATIKA MAKAZI HOLELA
Mara nyingi katika makazi haya, hua kuna tatizo la maeneno ya masoko na viwanda pia maeneo ya kufanyia biashara ndogondogo na kupelekea ongezeko la umasikinin katika makazi haya ingawaje kwa upande mwingine maeneo haya hukaliwa na watu wanye uwezo mkubwa kifedha na hua wanajenga majengo makubwa na ya thamani kubwa.
ATHARI ZA ONGEZEKO LA MAKAZI HOLELA
1. Kuongeza kasi ya umasikini kwa jamii husika kwa kukosa maeneo maalum ya kujishughurishia kazi zao binafsi za kiuchumi
2. Kuibuka kwa magonjwa ya kuambukiza kama vile kipindipindu na marelia kutokana na ukosefu wa maeneo ya kutunza taka ngumu na mifereji ya maji machafu
3. Kuikoseha serikali mapato yanayotokana na kodi ya ardhi ambayo mara nyingi hutolewa kwa uthaminishaji wa maeneo yalio pimwa
4. Uharibifu wa mazingira unaotokana na uvamizi wa maeneo yasio stahili kuishi binadam na hivyo kupelekea upotevu wa baadhi ya viumbe hai
5. Nchi kuwa na muonekanao mbaya usiovutia na hupelekea kuathiri utalii wa nje
6. Ukosefu wa maeneo ya biashra, viwanda na masoko hupelekea nchi kukosa wawekwzaji wa nje
7. Kuzuka kwa migogoro ya ardhi inayo sababishwa na tatizo la kutokua na mipaka inayotamburika( plot boundary conflict)