Real Estate(miliki) nchini Tanzania ni sekta inayokua kwa kasi sana
kulinganisha na miaka ilio pita, kufikia mwaka 2016 ongezeko la nyumba 200,000
huhitajika kwa mwaka na hii inasababishwa na ukuaji wa idadi kubwa ya watu
ambao wana kadiriwa kufikia milioni 45, hata hivyo kwa taarifa zilizo tolewa na
taasisi mbalimbali zinazojihusisha na uboreshaji wa makazi nchini zinaonesha kua
kuna hitajiko la nyumba zaid ya million 3, pamoja na juhudi kubwa sana zinazofanywa na
serikali ya jamhuri ya muungano wa Tanzania, lakini bado kuna uhitaji mkubwa wa
nyumba za makazi na biashara.
Kufuatia ongezeko hilo la mahitaji, Taasisi, mashirika na
makampuni ya umma na binafsi yanayojihusisha na
uwekezaji ya ndani na nje ya nchi yameonesha uhitaji wa kuekeza kwenye
sekta ya real estate (miliki) kwa kiasi kikubwa sana, mfano wa taasisi hizo ni
zile za mafao ya jamii kama PSPF, NSSF, PPF, LPF, GEPF ambazo zote hizo
zimewekeza katika sekta hii na kuonesha dalili ya kutaka kutatua tatizo la
uhitaji wa makazi yapatao nyumba 200,000 kwa mwaka 2016. Lakini pia wawekezaji Zaidi wanapewa
fursa ya kuendeleza sekta hii changa ya real estate katika mikoa yote nchini
SOKO LA REAL ESTATE TANZANIA
Kulingana na ukuaji na ongezeko la fursa mbalimbali za
kibiashara katika majiji mbalimbali nchini, soko la real estate kwa maana
nyumba za kuishi na zile za kibiashara zimezid kuongezeka siku hadi siku na hii
ni fursa kwa sekta binafsi kuongeza juhudi katika uwekezaji wa sekta hii ambayo
faida yake ni ya kudumu.
FURSA KWA VIJANA NA
WAHITIMU WA CHUO
Sekta hii sasa imekua ikiendeshwa na watu wasiokua na
utaalam nayo wanaofahamika kama “madalali” ambao kwa namna moja au nyingine
wamekua wakisababisha migogoro mikubwa katika jamii kutokana na ufahamu mdogo
wa sekta hii, hivyo basi kulingana na uhitaji wa wataalam wa sekta hii katika
jamii, kwa wahitimu wa vyuo wa sekta ya real estate ni muda muafaka sasa kuanza
kutoa huduma hii kwa kuunganisha wamiliki wa nyumba za makazi na za biashara
wahitaji wa nyumba hizo na upo uwezekano mkubwa wa kuanza kutoa huduma hii bila
kua na mtaji au kua na mtaji mdogo kabisa.
“usikose kufuatilia Makala
zangu katika mtandao huu ili kujua namna ya kuanza kutoa huduma za real estate
bila kuwa na mtaji au kuwa na mtaji mdogo, ukakuza kipato chako kwa muda mrefu”
Toa maoni yako hapa


